tangazo

Friday, March 18, 2011

IDARA YA UTUMISHI NA UTAWALA

IDARA YA UTUMISHI NA UTAWALA

UTANGULIZI

Idara ya utumishi na utawala  ni idara inayohusika moja kwa moja na usimamizi wa rasiliamli watu na kuhakikisha idara nyingine zinapangiwa watumishi kulingana  na Ikama  ya idara husika.

Halmashauri ya Manispaa  Bukoba ina jumla ya watumishi wapatao 1,205 kati  ya hao  watumishi 1148 wameajiriwa katika masharti ya kudumu na watumishi 57 ni watumishi wa muda (vibarua)

Idara ya utumishi ni idara mtambuka ambayo inahusika kupanga na kuandaa bajeti ya mishahara  ya watumishi  na kuhakikisha watumishi wanapata haki zao.

SHUGHULI ZINAZOFANYWA  NA IDARA

Baadhi ya majukumu yanayotekelezwa na idara hii ni pamoja na

i)             Kupandisha watumishi vyeo  kwa kushirikiana na bodi ya ajira na TSD Wilaya kwa upande wa walimu.

ii)           Kuthibitisha  watumishi kazini kwa kushirikiana na bodi ya ajira.

iii)          Kusimamia zoezi  zima la ujazaji wa fomu za OPRAS yaani upimaji wa kazi kwa watumishi

iv)          Kusimamia sheria, kanuni, zinazohusu watumishi

v)           Kushughulikia malipo kwa watumishi wanaostaafu kazi, mirathi na stahili nyingine.

vi)          Kuandaa mpango wa mafunzo kwa kupitia (TAA) Training Need  Assesment

Pamoja na kazi nyingine hizo ni baadhi ya kazi zinazofanywa na Idara hii.

CHANGAMOTO

i)             Bajeti  finyu ya mafunzo inayopelekea kutopatikana  fursa  ya kutosha  kwa watumishi  kwenda kwenye mafunzo

ii)           Upungufu wa watumishi hususan Idara ya Elimu, Afya  na kilimo.

iii)          Ukosefu wa vitendea kazi hususan kwa watendaji wa Kata na Mitaa.

iv)          Ukosefu na uelewa wa kanuni na sheria zinazohusu watumishi kwa  watumishi wenyewe.



Magedi Magezi,

Kaimu: Afisa Utumishi na Utawala

MANISPAA BUKOBA.

No comments:

Post a Comment